.

.

NYUMBANI KWA MISSY TEMEKE ALIVYOMUANDALIA BALOZI MWANAIDI MAAJAR(FAREWELL PARTY) PARTY YA KUMUAGA

Gallery

Posted by kifesi |
Posted by kifesi |
Kampuni ya Apple imezindua bidhaa mpya ya saa za mkononi ya kisasa ‘smart watch’ inayoitwa iwatch ikiwa ni bidhaa ya kwanza kutambulishwa na kampuni hiyo tangu alipofariki muanzilishi wa kampuni hiyo, Steve Jobs.
Saa hiyo imetajwa kuwa na matumizi mengi kwa mtumiaji wa kisasa anaendana na teknolojia huku ikimrahisishia maisha kwa kiasi kikubwa hasa katika kufahamu kinachoendelea duniani na afya yake.
Saa hiyo ya iwatch ina uwezo wa kumonitor mapigo ya moyo ya mtumiaji na hali yake ya afya na kumtumia maelezo sahihi huku ikimchorea taswira ya shughuli mbalimbali anazofanya kila siku.
iWatch ina uwezo wa kupima miondoko ya mwili wa mtumiaji kwa ujumla hivyo kuwa kama mshauri wa karibu katika masuala ya afya ya mtumiaji na kazi mbalimbali anazozifanya.

Pia, mtumiaji anaweza kutumia Wi-Fi na GPS hivyo anaweza kupata vitu ambavyo anatumia kwenye computer yake ya (Mac) au iphone  na anaweza kuchagua picha na miziki kupitia saa hiyo yenye speaker zisizoharibika kwa kuingiliwa na maji.

Simu hiyo inatarajiwa kuingia sokoni mapema mwaka kesho na kwa mujibu wa mtandao wa ipadvisor wa Uingereza, saa hiyo itaanza kuuzwa Marekani kwa kiasi cha $349 (580,561 za Tanzania).
Mkurugenzi wa kampuni hiyo amesema malipo yatafanyika kwa njia/huduma mpya waliyoianzisha inaitwa ‘Apple Pay’.
Apple iWatch ina sura zaidi ya 11 na mtumiaji atakuwa na uwezo wa kubadili mikanda kadiri apendavyo.

Kampuni ya Apple mezindua pia simu zake mbili mpya ambazo ni kubwa ikilinganishwa na simu zake za awali. Screen ya iPhone 6 ina upana wa nchi 4.7 huku iPhone 6 Plus ikiwa na screen yenye nchi 5.5.
iWatch imechukuliwa kama mshindani mkubwa wa Rolex iliyokuwa imeteka soko.
Posted by kifesi |
Wimbo Mpya: Yemi Alade- Kissing
Posted by kifesi |
Mwimbaji Justin Bieber amejitoa ufahamu wakati akiwa katika show ya mitindo iliyokuwa ikirushwa Live kwenye TV, Jumanne, September 9  na kuchojoa nguo mbele ya kadamnasi.
Bieber alifika jukwaani ambapo watu wengi walihudhuria, na alipofika alimwambia Lara Stone kuwa hajisikii huru hadi avue nguo zote.
Sekunde chache baadae alianza kuvua nguo moja moja hadi alipobaki na nguo ya ndani pekee aka boxer.
 Picha: Justin Bieber achojoa nguo jukwaani

Show iliendelea na Bieber alionesha mwili wake akiwa ndani ya vazi hilo la ndani tofauti na matarajio ya wengi na Lara Stone aliendelea naratiba kwa kumpandisha jukwaani Rita Ora.
Posted by kifesi |















https://scontent-b-cdg.xx.fbcdn.net/hphotos-xpa1/v/t1.0-9/p417x417/1380420_659538917403133_1569513863_n.jpg?oh=1a4a9ef06b107950819d8c72beacd9bc&oe=548A417Fhttps://scontent-b-cdg.xx.fbcdn.net/hphotos-xpa1/v/t1.0-9/p417x417/1380420_659538917403133_1569513863_n.jpg?oh=1a4a9ef06b107950819d8c72beacd9bc&oe=548A417F
















































Posted by kifesi |
http://www.timesfm.co.tz/content/uploads/2014/9/10/cache/Mwanamke%20ateswa_full.jpg
Mwanamke mwenye umri wa miaka 25, raia wa India ameokolewa na polisi baada ya kufungiwa bafuni na mumewe kwa muda wa miaka mitatu akiteswa kwa sababu tu alijifungua mtoto wa kike! Pamoja na mateso ya kunyimwa chakula mara kadhaa, mwanamke huyo alizuiwa kumuona mwanae huyo kwa kipindi chote cha miaka mitatu. Kwa mujibu wa gazeti la International Business Times, Afisa wa polisi aliyetajwa kwa jina la Seema Kumar ameeleza kuwa mwanamke huyo alikutwa akiwa amedhoofu na baada ya kutolewa nje hakuwa na uwezo wa kufungua macho vizuri katika sehemu ya mwanga kutokana na giza alilolizoea kwa kipindi cha miaka mitatu bafuni. Seema amesema mwanamke huyo aliwaeleza polisi kuwa hata wakwe zake (wazazi wa mumewe) walimchukia na hii ilichochewa zaidi na kiasi kidogo cha mahari aliyotoa ili kufunga ndoa ya mumewe huyo na kwamba siku zote walikuwa wakimtaka aongeze kiasi hicho. Kwa utaratibu wa baadhi ya makabila ya kihindi mwanamke ndiye anaelipa mahari. Uchunguzi wa polisi umebaini kuwa tangu mwanamke huyo afunge ndoa na Prabhat Kumar Singh mwaka 2010 amekuwa akiteswa mara kwa mara na mumewe huyo huku wakwe zake wakimtaka kuongeza mahari na kumsakama kwa kujifungua mt
oto wa kike.