.

.

NYUMBANI KWA MISSY TEMEKE ALIVYOMUANDALIA BALOZI MWANAIDI MAAJAR(FAREWELL PARTY) PARTY YA KUMUAGA

Gallery

Posted by kifesi |

Daktari mmoja bingwa wa saikolojia, Erick Mutchumbh, amesema tabia zinazofanywa na nyota wa muziki, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ zinaashiria kuwa ni mgonjwa aliyeathirika kisaikolojia na matatizo ya unyanyaswaji wakati wa utoto wake.

Mutchumbh alitoa maelezo hayo baada ya kuombwa kuzungumzia tabia za Shilole za kugombana mara kwa mara na mpenzi wake, Nuh Mziwanda, kama zinaweza kuwa ni tatizo la kisaikolojia linalomsumbua mmoja wao au ni ugomvi wa kawaida wa kimapenzi.

“Mtu yeyote aliyepitia matatizo hasa unyanyasaji akiwa mtoto ‘child abuse’ iwe kunyanyaswa kwa kubakwa, kupigwa, kunyimwa chakula au mateso ya aina hiyo, akikua bila kupata tiba ya kisaikolojia huwa na tatizo kubwa kwa miaka mingi akiwa mtu mzima.

“Miongoni mwa matatizo hayo ni pamoja na kupenda kujitenga, hasira za karibu, tabia za ajabu na kubwa zaidi ni kumfanyia mtu mwingine hasa mtoto ukatili aliofanyiwa yeye kitaalamu wanaita ‘Propensity Victimization,’” alisema daktari huyo.

Alisema katika nchi zilizoendelea, tatizo hilo hupewa kipaumbele katika matibabu kuliko ilivyo kwa nchi nyingi za kiafrika kwani madhara yake huwa ni pamoja na mwathirika kuamua kujinyonga au kuua.

Kwa maelezo hayo, mengi yanaonekana kufanana na matukio yaliyowahi kumkuta Shilole, kwani akiwa na umri wa miaka 14, aliwahi kubakwa, pia anatajwa kujihusisha kimapenzi na watu wenye umri mkubwa, ikiwa ni pamoja na kufanya kazi ngumu katika umri mdogo.
Posted by kifesi |
chris-brown-rihanna-665x385
Kwenye intervew aliyofanyiwa hivi karibuni msanii wa rnb Rihanna anasema alishtuka kusikia Chris Brown anamtoto mwenye miezi nane. 
Hollywood
 Life imeripoti kuwa Rihanna amemtakia mema Chris kwenye maisha ya kuwa baba na anauhakika Chris atakuwa baba mzuri kwa mtoto wake wa kike.