.

.

NYUMBANI KWA MISSY TEMEKE ALIVYOMUANDALIA BALOZI MWANAIDI MAAJAR(FAREWELL PARTY) PARTY YA KUMUAGA

Gallery

Posted by kifesi |
rambo

Polisi nchini Canada wanamsaka mtu hatari mwenye silaha ambaye amevaa mavazi kama ya muigizaji wa filamu za mapigano Rambo. Mtu huyo amewaua kwa kuwapiga risasi maafisa watatu wa polisi na kujeruhi wengine wawili katika tukio hilo la pamoja. Mashambulizi hayo ya risasi yamefanyika wakati polisi walilipokea simu juu ya mtu aliyekuwa na silaha Kaskazini mwa mji wa Moncton katika Jimbo la Pwani ya Mashariki ya New Brunswick.  Maafisa hao watatu waliokwenda katika eneo hilo waliuwawa na wengine kupata majeraha lakini sasa wapo katika hali nzuri. Mtuhumiwa huyo mwenye umri wa miaka 24 Justin Bourque, kutoka mjini Moncton, anadaiwa kuwa alibeba silaha nzito za mapigano pamoja na visu.Polisi waliweka picha ya mwanaume huyo akiwa amevaa mavazi ya kijeshi na kushika bunduki.

0 comments:

Post a Comment