.

.

NYUMBANI KWA MISSY TEMEKE ALIVYOMUANDALIA BALOZI MWANAIDI MAAJAR(FAREWELL PARTY) PARTY YA KUMUAGA

Gallery

Posted by kifesi |
Mara nyingi wengi wetu tumekuwa tukiumiza hisia za wenzi Wetu bila kujua. Kumuumiza mtu mwingine kihisia ni ile hali ya kusababisha emotional discomfort kwa mtu mwingine kiasi cha kumfanya apoteze furaha yake. Haya ni baadhi ya mambo yanayoweza kupunguza hali tajwa hapo juu:

1.Jaribu kuwa na mtazamo chanya (positive attitude) juu yake. Mara nyingi mitizamo hasi juu ya mtu mwengine huweza kusababisha umuelewe tofauti mwenzio hata kama tendo alilolifanya yeye ni la kawaida tu hata kama angekuwa amelifanya mtu mwengine. Ila kwa vile tu amefanya yeye na tayari una mtazamo hasi kwake basi utamuelewa"kutokumuelewa".Hii itapelekea kumuumiza!

2. Don't be too demanding. Hili kwa wana ndoa ni chanzo sana cha kuumizana kihisia.Unapojiona una haki ya kufanyiwa kila jambo hapo ni mwanzo wa kukwazana na kuumizana kihisia. Mfano, mwanamume unapoona siku umeamka na bado shati halijanyooshwa, na mwenza wako anafanya majukumu mengine, jifunze kujihudumia na acha kulalamika kuwa hujaliwi.

Halikadhalika kwa kina dada usimgeuze mumeo "ATM " au "Punda wa kukodi" ukamtishwa kila aina ya majukumu, hata yale ambayo ungeweza kujifanyia mwenyewe matokeo yake ni mmoja kuona hawi appreciated na mwenzake na hii itamuumiza sana kihisia

3. Jifunze kuwa msikivu(good listener) na maintain eye contact pale unapoongea na mwenza wako Mara nyingi mtu unapozungumza unapenda usikilizwe, haipendezi unapoongea na mtu halafu akawa anafanya mambo mengine, utahisi umedharauliwa. 

4. Usichoke kumsoma mwenza wako. Waswahili wanasema ukimjua mbwa jina hakusumbui. Jaribu kumsoma mwenza wako na kumjua vizuri ,hii itasaidia kupunguza kumuumiza kihisia kwa sababu utajua nini ufanye na kwa wakati gani. Learn to understand his/her mood. Unaweza ukacheka mahala ambapo yeye alitarajia uoneshe huzuni ikasababisha kutoelewana na kuhisi kuwa umeshindwa "kuvaa viatu vyake"

5.Learn to let it go. Jiepushe kuweka vinyongo na visasi. Mara nyingi watu huumizana kihisia kutokana na migogoro ambayo haitokani na mgogoro ulioibuka kwa wakati huo(imediate cause) bali hutokana na yale yaliyorundikana mda mrefu(basic causes), hivyo immediate causes huwa sababu tu ya "kuwasha moto".achana na ule msemo "ukimwaga mboga namwaga ugali"

6.Usiwe mjuaji sana. Kuna watu wengine yani yeye hujifanya ni mjuaji wa kila kitu na kila asemalo au afanyalo mwenzie basi hajui au amekosea. Hii inakwaza kwa mwenza wako, na humfanya ahisi unamdharau na huheshimu maoni yake au kile afanyacho.

7.Onesha upendo kwake, usiishi kwa mazoea. Unapoonesha upendo kwake unakuwa unafanya uwekezaji mahaba juu yake na humuondoshea madoa ya yale uliyomfanyia katika makosa. Usiwe wewe ni receiver kila siku, jitahidi nawe uwe giver katika kuonesha upendo. Hapa sizungumzii pesa ,nazungumzia kuonesha upendo.

Mfano:Isiwe kila siku wewe ndio wa kuitikia "i love u too", "I miss u too", jenga utamaduni wa ushindani kuwa wewe ndio uwe wa kwanza kusema kila siku na sometimes mtanie kuwa umemshinda ili na yeye nae kesho ajitahidi awe wa kwanza just make it as a 
funny
 game lakini inaboresha ndoa yenu.Hili ni muhimu mno na ndio mana nimeliweka mwisho ili mlikumbuke sana.

8.Ongezea

0 comments:

Post a Comment