Baada ya Polisi kusimamisha gari walitaka Jamal aonyeshe kitambulisho chake lakini hakuwa nacho kwa wakati huo ambapo baadae walimtaka ashuke kutoka kwenye gari lakini Jamal akakataa ndipo Polisi wakaamua kuvunja kioo cha upande wa mlango alipokua amekaa Jamal na kumchukua.
Watoto wawili waliokua wamekaa nyuma ya gari waliumia baada ya kurukiwa na vipisi vya kioo kilichovujwa ambapo video ya tukio lote ilichukuliwa na mtoto Joseph aliekua amekaa kiti cha nyuma akiwa na mdogo wake wa kike mwenye umri wa miaka 7 ambae ndio alilia sana baada ya Jamal kuvunjiwa kioo na kuchukuliwa.
Polisi waliohusika kwenye hili tukio wamesema walichukua maamuzi hayo pia baada ya kuona kulikua na hatari ya wao kushambuliwa sababu walimuona Jamal kama anajiandaa kufanya kitu flani walichohisi kinaweza kuwa ni kuwashambulia.
CRDT-MILLARDAYO
0 comments:
Post a Comment